KANISA KWA LEO
7.1. MAANA YA NENO « KANISA» NI NINI?
Neno la kiyunani «ecclésia» maana yake ni «kuitwa inje ya». Kanisa haina uhusiano na dunia. Liko la mbinguni, linaitwa inje ya dunia kwa kukuwa lake Kristo.

7.2. KANISA NI NINI ?
Neno la Mungu linajua kanisa moja tu. Ile kanisa inaundwa na waamini wote. Waliunganishwa pamoja kuwa mwili mumoja, hapana kwa kukuwa mwana memba wa shirika lakini kwa Roho Mutakatifu (1 Wakor 12 :13 na Waef 1 :23).

7.3. KANISA LINAANJA WAKATI GANI ?
Kanisa linaanja siku ya pentekoste, siku 50 nyuma ya kufufuka kwa Bwana, mbele ya saa 3 ya asubui (Matendo 2, shairi 15 kwa upeke).
- Sababu gani hapana mbele?
Kanisa halingeweza kuanja mbio sana, kwa sababu Kristo alipashwa kufa, kufufuka na kutukuzwa mbele Roho Mutakatifu aweze kukuja (Yoani 7 : 37-39). Ndani ya Mathayo 16 lingali kwa wakati unaokuja : “ juu ya mwamba huu nitajenga kanisa langu “ (shairi 18).
- Sababu gani hapana nyuma?
Kanisa lingepashwa kuwa limeanja siku ya pentekoste ndani ya Matendo 2, kwa sababu tunasoma kwa mwisho wa sura ile kwamba «Bwana alizidisha kila siku kwa wale waliokuwa wakiokolewa». (Tafadhali 1 Wakor. 12 : 13).
7.4. KANISA LINAFUNULIWA NDANI YA AGANO LA KALE ?
Hapana. Siri ya Kristo na ya kanisa haikukuwa bado «na funuliwa» mupaka pale (Waef 3 :5). Ilikuwa kazi ya mutume Paulo kuitangaza (Waef 3 :2,7,8). Agano la kale linataja tu mifano ya kanisa (kwa mufano Rebeka) lakini mutu hawezi kutambua ukweli wa kanisa kwa hizi picha – bila mwangaza wa Agano Jipya.

7.5. NI WANANI WANAUNDA KANISA LA LEO ?
Ni wote wenye wanaoamini habari njema ya wokovu wao (Waef 1 :13) – kutoka wayuda na wamataifa – na wanaungana namna hii kwa mwili mumoja (1 Wakor 12 :13).
7.6. NAMNA GANI KUKUWA MUSHIRIKI ?
Ni sawa, hakuna kitu cha kufanya. Kama uko mwamini, ulishakuwa kiungo cha „kanisa la Mungu aliye hai“, kanisa moja linalojulikana ndani ya Agano Jipya. Halina nia ya „kuunga“ mutu hata awe nani. Mwamini wa kweli ni kiungo cha mwili wa Kristo (1Wakor 12:12).

7.7. SABABU GANI AGANO JIPYA INATUMIA PICHA KWA KUONYESHA KANISA?
Namna gani unaweza kufasiria mumbute anayeishi ndani ya mwitu wa equator – mwenye hayaonaka gari ya mabawa na hajui kama ni nini? Hakika inaomba kutumia picha, kwa mfano kusema kama gari ya mabawa ni ndege kubwa, lakini ya chuma, yenye haiwezi kutua juu ja miti, na inakunywa mafuta na kazalika. Ile inaweza kuleta ufahamu kwa mumbute jinsi gari ya mabawa iko. Na kwa namna sawa Mungu alitumia vitu vyenye tunazoea (mwili, bibi, nyumba) ili kwa kutufasiria jinsi kanisa liko.

7.8.a. WANATAKA KUSEMA NINI KANISA NI MWILI WA KRISTO?
Hivi wakati Mungu anaonyesha kanisa kama mwili, ile inatuonyesha (i) kwamba tuko wote tofauti kama viungo vya mwili na tuna kazi mbalimbali na kwamba (ii) kuna umoja, kweli sawa viungo vya mwili vinatumika pamoja ndani ya umoja. Na, ya muhimu sana, Kristo ndiye kichwa ao mkubwa wa mwili huu.

7.8.b. WANATAKA KUSEMA NINI KANISA NI NYUMBA YA MUNGU?
Ndani ya nyumba vyote vinatengwa kwa namna ya kupendeza bwana wa nyumba. Hivi ndani ya nyumba ya Mungu :Utaratibu fulani ni wa kuheshimiwa (1 Tim 3 :15). Ndani ya nyumba ya Mungu, utukufu unapashwa kupewa Yeye (Zaburi 93:5)

7.8.c. WANATAKA KUSEMA NINI KANISA NI BIBI YA KRISTO ?
Bibi ana uhusiano pamoja na mapendo. Picha inatuonyesha kwamba kuna uhusiano wa mapendo kwa Kristo na kanisa (Waef 5:25). Mapendo ya kanisa haipashwi kugawanywa lakini inapashwa kukuwa kwa Kristo peke yake (2Wakor 11:2). Na bibi ana hamu kubwa moja tu : kwamba Bwana akuje! Amina, uje Bwana Yesu (Ufunuo 22:17,20).

7.9. TUNATAKA KUSEMA NINI, KUSEMA “KANISA LA MUNGU PA «X,Y,Z»?
(1e) kanisa la Mungu pahali fulani (tuseme la Pekelele) linaundwa na waamini wote wa Pekelele. Ile iko sehemu ya kanisa la Mungu (uone swali la pili).
(2e) siku zilizopita (kwa wakati wa Agano Jipya), ile ilikuwa raisi kwa kuona kwa sababu wakristo walikusanyika pamoja fasi moja. Walikuwa na najulikana. Hata musiamini mumoja hakupima kujiunga nao (Matendo 5: 13). Kama walikuwa wengi kwa kukusanyika fasi moja, walipatikana ndani ya nyumba mbalimbali, lakini walitenda kwa ushirika wamoja pamoja na wengine.
(3e) leo, mambo yamekuwa magumu zaidi (lakini misingi ya Mungu inadumu). Watu wameunda makanisa, mashirika, mazehebu, na kazalika, wakiingiza hitaji ya kukuwa mushirika (mbali na mushirika wa mwili wa Kristo). Hivi tunaweza ‘kuona’ namna gani ao
‘kuonyesha’ kanisa la Mungu pahali fulani kwa leo? Moja tu ni kwa kukusanyika juu ya musingi wa maandiko pamoja na wote wenye kuwa tayari kwa kufanya hivi vilevile - lakini bila kusahau kwamba wenye wanakusanyika hivi hawaunde hakose kanisa lote kwa pahali fulani.
(4e) kanisa la pahali linaleta ushuhuda ya pahali ya kanisa – ambalo liko la ulimwengu.

7.10. “KUKUSANYWA KWA JINA LAKE“ MAANA YAKE NINI?
Mwamini anataka kufanya yote kwa jina la Bwana, hata kukula na kukunywa (Wakol 3: 17). Lakini kama tunataka kukusanyika kwa jina lake (Mathayo 18 : 20), Bwana anapashwa kuwa shina ya makutano, na anaweza kuongoza yote na kukuwa shina la angalisho yetu. Inawezekana kukusanyika kwa jina la Bwana kama inatambulikana mamlaka yake. kwa ufupi :
- Pahali – fasi ya Mungu
- Wawili ao watatu – hesabu ya Mungu
- Wanakusanywa – nguvu ya Mungu (nguvu ya Roho Mutakatifu)
- Wanakusanyika – umoja wa Mungu
- Kwa jina lake – jina la Mungu
- Niko pale - kuwepo kwa uutu wa Mungu
- Katikati yao – shina la Mungu

7.11. KUSANYIKO LA KANISA NI NINI?
Ni kusanyiko pale «kanisa yote» inakusanyika pamoja (1Wakor 14: 23), «kama kanisa» (1Wakor 11 : 18). Wakati tunasema kanisa yote, inasikika wazi kwamba ni wale ambao wanaweza na wana hamu ya kulifanya. Agano Jipya inaleta kwa uchache sababu 3 kwa kusanyiko za kanisa namna zile :
7.12. NI NANI ANAONGOZA YA KUSANYIKO?
Wakati waamini “wanakusanywa kwa jina lake“ (Mathayo 18: 20) sasa pale Kristo anapashwa kuwa shina. Anaongoza yote. Haiko kusanyiko yenye inaongozwa na mutu. Kristo anaongoza na Roho Mtakatifu anaongoza “sawa inamupendeza“ (1Wakor 12:11). Kuna uhuru kwa kila ndugu (hata hivi wanawake wanapashwa kunyamaza ndani ya makanisa (1Wakor 14: 34)) kwa kusaidia: kutaja wimbo, kuomba, ao kusema kwa kujenga (1Wakor 14: 26-33).

7.13.
Kwa “kazi ya Neno” (Matendo 6: 4) tunawaza juu ya mafundisho na mahubiri ya Neno la Mungu kwa waamini. Ile ingepashwa kufanywa na wenye ambao walipokea zawadi juu ya ile (waalimu na wachungaji). Kazi hii inaweza vile kukuwa na hali ya unabii : Neno la Mungu linaweza kwa zamiri ya taifa la Mungu. Neno la Mungu halitambui makanisa pamoja na musingi « mutu moja afanye yote ». Pa Antiokia, kulikuwa « manabii na waalimu » (hapana « muchungaji », Matendo 13 : 1). Paulo anasema na wakorinto : « Basi nini, ndugu zangu ? wakati munapokutana, kila mumoja ana zaburi, ana mafundisho …maneno yote yafanyike kwa kusudi la kujenga » (1Wakor. 14 : 26). Vile, yote inapashwa kutendeka katika mapendo ndani ya woga mutakatifu inayotoka kwa uwepo wa Mungu.

7.14. KUNA UMBALIMBALI GANI KATIKATI YA ZAWADI NA KAZI (HUDUMA)?
Zawadi ni uwezo kiroho (zawadi ya ualimu, uinjilisti, na kazalika). Kazi ndizo mapaswa ao jukumu sawa watumishi ao waangalizi. Zawadi ni kwa mwili mzima wa Kristo (Waef 4: 12) hivi mwalimu, kwa mufano anaweza kufundisha katika miji na inchi zingine) lakini kazi zinaletwa kwa pahali : „Waangalizi kwa kila muji „ (Tito 1: 1) na „ chunga kundi la Mungu lililo kwenu“ (1Petro 5: 2).

7.15. KWA SABABU GANI HATUTAJE WAZEE?
Ndani ya Agano Jipya, wazee walitajwa kila mara na mitume (Matendo 14: 23) ao na mawakili (wajumbe) wao (Tito 1: 5) ambao waliagizwa na mitume kwa kuifanya. Leo hakuna tena mutume (maana walipashwa kuwa waliona Bwana, Matendo 1: 22 na 9: 4,5). Hivi hakuna tena wajumbe wa mitume tena ambao wangeweza kuteua. Lakini kuna tena watu ambao wana alama zinajotajwa kwa wazee (1Timot. 3: 1-6). Lakini usomi wa majina ya alama hizo inaonyesha kwamba watu namna wale ni wachache sana. Lakini wale ambao wana alama hizo wanaweza kufanya tena kazi ya muzee (1 Petro 5: 2, Matendo 20: 28).

7.16. NI ZAWADI GANI AMBAZO ZIKO NDANI YA KANISA?
Zawadi tano muhimu zinatajwa ndani ya Waefeso 4: Kristo alitoa :
- Mitume – watu ambao waliona Bwana (Matendo 1: 22 na 9: 4 na 5).
- Manabii – wale waliotabiri (walileta Neno la Mungu kwa watu. Mbele Agano Jipya iishe, manabii walifunuliwa (Waef 3: 5). Kwa leo Biblia, ufunuo, imeisha. Lakini kuna tena kazi ya unabii : Neno ambalo linatoka kwa Mungu kwa wakati muzuri,likiwa na msingi wa Neno lake, kwa kujenga (1Wakor 14). Kulikuwa vile wanawake wenye walitabiri (Matendo 21: 9) – kwa sehemu yao, hapana ndani ya kanisa (1Wakor 14: 34).
- Wainjilisti – wanaoleta injili kwa watu waovu, wapotevu (Matendo 21: 8).
- Wachungaji – wanaonyesha usafi wao kwa watu kama mchungaji anasafisha kondoo ya kundi lake (leo watu wamesikia kitu kingine kwa “ muchungaji “ – aina ya mutu ambaye anafanya yote. Haiko ule “ muchungaji “ wa Biblia).
- Waalimu – wenye kuwa na uwezo wa kuonyesha kweli ya Neno la Mungu kwa namna hata mioyo ya wenye kusikia iwake kwa kweli.
Kuna tena zaidi, zingine zawadi (1 Wakor. 12 na Waroma 12).

7.17.a. KAZI YA ZAWADI ZA MIUJIZA ILIKUWA NINI?
Juu ya nini Mungu alileta ? Juu ya uinjilisti ? Juu ya uonyesho wa kusisimua ? Juu ya kupunguza magumu ya waamini? Hapana, Mungu alileta alama za miujiza, juu ya kuonyesha kwamba Mungu ameleta wakati mupya. Wakati wa sheria ulikuwa umepita. Mungu alikuwa amefanya kanisa kwa Roho Mutakatifu. Vile, inawezesha wanafunzi wake siku ya pentekoste (mwanzo wa kanisa) kwa kuzungumuza lugha za kigeni zenye watu wengine waliweza kusikia. Ni nani angekana kwamba Mungu alikuwa kwa kazi? Lugha zilikuwa alama kwa wayuda peke yao (1Wakor 14:21). Kulikuwa vile uponyaji (Matendo 3), hapana kwa kupunguza magonjwa ya waamini lakini kama alama ya wasioamini (Matendo 4: 16, 30 na Waebrania 2: 4).

7.17.b. KAZI YA ZAWADI ZA MIUJIZA KWA LEO NI NINI?
Kengele za makanisa zinalia wakati kazi inaanza na hapana wakati inaisha, sivyo? Ni sawa vile kwa zawadi ya miujiza. Ni kweli Mungu anaweza kila mara kufanya miujiza kwa siku za leo, na anafanya. Lakini si sawa na kufanya zawadi. Na iko nini kwa lugha? Sawa, muniruhusu kuuliza : Munajua mutu mumoja peke yake anayeweza kusema lugha ambayo hayajifunjaka bado (maana ni ile ilijitokeza ndani ya Matendo 2).

7.18. MAANA YA «ANGUKO LA KANISA» NI NINI ?
Kwa uraisi leo mambo iko tofauti ya namna Mungu aliyafanya kwa mwanzo wa pentekoste. Wakristo wako sehemu sehemu ndani ya vikundi mbalimbali. Wengi wanakuwa wanamemba wa vikundi badala ya kufanya kwa uraisi kama kiungo cha mwili wa Kristo. Kuna ubaya wa kanisa (kazi ya mutu mumoja na kazalika) mafundisho mabaya (inaambatana na Kristo, kwa kuvaa mwili kwake, hali yake bila zambi, uutu wake, kazi yake, wokovu na kazalika). Uongozi kwa kinywa wa Maandiko iko naleta maswali. Ndani ya mahali ambapo ubaya wa zamiri unavumiliwa, ile inafanana kukuwa «juu ya musitari sawa kiviringo yenye inaelekea » kushuka chini … Kuna vile ukosefu (ao hata kutokukuwa) utengano na ubaya mahali mengi ndani ya wakristo.

7.19. NAMNA GANI TUNAWEZA KUONYESHA UMOJA KWA WAKATI WA KUANGUKA NA WA KUGAWANYIKA ?
Mutu aliharibu yote ? Ndio, lakini ile haiko kusema haiwezekane kutenda juu ya misingi ya Biblia. Kama watu wanafanya vikundi na kazalika, tunaweza hata hivi kufanya yenye Biblia inatuagiza. : Kujikusanya kando ya Bwana Yesu (Mathayo 18 : 20), kwa kuonyesha kwamba tuko viungo vya mwili wa Kristo (1Wakor. 12 :12, 13). Ombeni, na Bwana atawaonyesha waamini wengine ambao wanataka kumutambua kama Bwana. Kusanyikeni, pamoja nao mukipima mara ngapi itawezekana kutenda ile ambayo Biblia inafundisha. Ile haina maana kwamba kupima kuunda kanisa mupya. Mungu aliunda kanisa zamani na ile inatosha. Kwa leo, tuna uajibu wa kutambua kwamba alilifanya.

7.20. NI NANI ANAWEZA KUVUNJA MKATE ?
Sawa, ni mwamini yeyote – mwenye hayatupwa. Sababu gani kila mwamini ? Kwa sababu ni uhuru kwa kila kiungo cha mwili wa Kristo (1Wakor 10 : 17). Na maana ya «kutupwa» ni nini ? Namna gani ile inaweza kutokea ? Hivi, kuna sababu kubwa tatu :
- Ubaya wa zamiri : Mutu ndani ya 1 Wakor. 5 kwa mufano alipashwa “kutupwa inje”
- Mafundisho mabaya: Kama mutu halete mafundisho ya Kristo (2 Yoani 9- 11), haifai kumupokea ndani ya nyumba yako, tena hapana kukula chakula cha ukumbusho pamoja naye. Mafundisho mabaya ni chachu (Wagalatia 5: 9).
- Kujiunga na ubaya. Yule ambaye anasalimia mudanganyifu ndani ya 2Yoani 9- 11 anakuwa «mushiriki kwa matendo yake mabaya ». Wale ambao waliangalia hekalu ya sanamu pa Korinto waligeuka “washiriki wa meza ya mashetani” (hata kama hawaamini kwa sanamu wao wenyewe, 1 Wakor. 10: 19-22. Ona vile 1 Wakor. 15: 33, Ufunuo 2: 14).
7.21. NI UHUSIANO GANI KATIKATI YA MAKANISA YA PAHALI?
Kusanyiko la pahali (ao kanisa) iko sehemu ya kanisa mzima la Mungu (1Wakor 1:2). Kusanyiko za pahali zinatumika katika utaratibu wengine pamoja na wengine (kama viungo vya mwili wa mutu vinatumika pamoja bila kimoja kuchukia kingine). Wakati kanisa la pahali linakamata mpango (linaweka kwa mufano mutu chini ya hukumu ao linakubali mwamini kwa ushirika) ile inafanyika kwa makanisa zingine zote : « chochote mtakachofunga duniani kitakuwa kimefungwa mbinguni (Mathayo 18: 18). Paulo anarejea kusema kwamba maonyo ambayo analeta kwa wakorinto inafanyika kwa waamini wote pahali pote (1Wakorinto 1: 2; 4:17; 7: 17; 11: 16).
7.22. KUWEKWA CHINI YA HUKUMU YA KANISA NI NINI?
Lengo la hukumu ya kanisa ni kusaidia kwa kusimama tena kwa mutu ambaye anatenda kwa namna ambayo haiambatane na mafundisho ya kikristo. Namna ya hukumu ya kutumia inafatana na hali. Kuna aina saba mbalimbali :
- kujiachililia kwa kumatwa na kosa fulani fulani : Wagalatia 6 : 1-2
- kuonya na kujihazari / kutaja mojamoja yenye haiko sawa : 1Watesal 5 : 14 ; 2Watesal. 14 : 15.
- kukemea mbele ya watu wote : 1Timoteo 5 : 20 ; Wagalatia 2 : 11-14.
- kumukataa / kumwangalia mutu wa mafundisho mabaya na mutu mjushi: Tito 3 :10-11, Waroma 16: 17.
- hukumu ya kunyamaza kimya : 1Timoteo 1: 3-4, Tito 1: 10-11.
- kosa la kibinafsi : Mathayo 18: 15 na kazalika.\
- kuondoa : 1Wakorinto 5: 13.

7.23. UJUSHI (secte) NI NINI ?
Kwa ufupi : Ni wakati mutu anakuwa mwana memba wa (zehebu ao shirika). Ingine bila kukuwa k iungo cha mwili wa Kristo, ni muhimu ili kupokelewa ndani ya ushirika wa kikristo.

7.24. TUKO ZEHEBU ?
Kama tunapatikana ndani ya zehebu (ao shirika na jina), ya muhimu ni kutoka ndani. Wakristo wa kwanza hawakukuwa na jina na sisi hatuna hamu nayo vile kwa leo. Tunaweza kukuwa na furaha kwa sababu ya kukuwa viungo vya mwili wa Kristo.

7.25. NAMNA GANI TUNAPASHWA KUJIWEKA VIDI YA WAKRISTO WENGINE WENYE HAWAKUSANYIKE PAMOJA NASI ?
Wako ndugu na dada ndani ya Kristo. Hatuwezi hakose kutembea nao (kuvunja mkate pamoja nao) lakini tunawapenda. Namna gani kuwaonyesha mapendo ile? kwa kutafuta vitu vyao? kwa kujaribu kukuwa msaada kwao kwa namna ya undugu, tukitafuta kuwajenga ndani ya imani yao. Hii inaingiza kila mara kwa kujifunja mafundisho kutoka Neno la Mungu.

7.26. NI YA WAPI ILIYO YA LAZIMA : KUKUWA VEMA KWA NGAMBO YA MAFUNDISHO AO KUKUWA MUTIIFU KWA BWANA?
Haina faida kulinganisha moja na ingine. Tunahitaji yote mbili ! mafundisho bila utii ni sawa mifupa ya mwili bila nyama na utii bila mafundisho ni sawa mwili bila mifupa yenye inaweza kuisaidia isimame !
MASWALI ZINGINE :
Kuna uhusiano gani katikati ya kanisa na ukristiano wa sasa, ni kusema ufalme wa Mungu na ufalme wa mbinguni? Ushuhuda wetu kwa leo ni nini? kwa saa hii kanisa ni wapi? Namna gani Roho Mutakatifu anatumika ndani ya kusanyiko ? Sababu gani tunavunja mkate kila juma ? Juu ya nini tunakusanyika siku ya yenga ? Kazi ya kanisa duniani ni nini ? Mafaa yake ni nini ?
